Monday, July 20, 2015
SITASAHAU MAISHANI.
Nilikuwa darasa latano
kipindi hicho, nilikuwa mimi na wadogo zangu wawili. Kawaida yetu
ilikuwa kila tukimaliza kula chakula cha usiku tunapumzika kidogo,
halafu tunasali, na kama kuna mwenye homework anafanya na anaingia
kitandani na kulala. Sikuhiyo baba alikuwa hajarudi kipindi nafanya
homework baada ya kuwa tumemaliza kusali na mama pamoja na wadogo zangu
walikuwa tayari wamesha lala. Takribani saa sita usiku baba akarudi
akiwa chakali amelewa, alibisha hodi mama akaamka na kumfungulia,
alikuwa mkali sijawahi kumwona baba yangu akiwa mkali vile, akamnasa
mama makofi mbele yangu, mama aligumia kwa maumivu, hali ile iliniuma
sana mpaka nikalia. Hakuishia hapo bali alimrushia mateke kana kwamba
anapigana na mwanaume mwenzake. Mama aliumia sana, nami sikuweza
kuvumilia haliile, kipindi hicho tulikuwa tumeagizwa fimbo za kupeleka
shuleni aina ya mikamilwa, nilichukua fimbo mkamilwa mmoja nikamfuata
baba aliyekuwa amemwangusha mama chini nakuendelea kumpa makonde
yasiyonaidadi. Kwahasira na nguvu nilimtiririshia baba mvua za fimbo
mgongoni mpaka nayeye akapiga mayowe. Akamwacha mama na kuanza
kunikimbiza, kwakuwa mlango ulikuwa haujafungwa nilitoka mbio nayeye
yupo nyuma yangu anakuja mbio anikamate, nikakimbilia sehemu moja
iliyokuwa imezibwa njia kwa miiba ya michongoma. Kwakuwa sehemu ile
nilikuwa naijua nikairuka miba ile nayeye hakuwa akijua kama kuna miba,
aliingia mzimamzima. Alikipata hakika. Nikahamia kwa rafiki yangu wiki
nzima na mama akawaomba wazee watusuluhishe mimi na baba. Nilimwomba
radhi baba na akanisamehe. Je nisingechukua maamuzi magumu kama hayo
mamaangu siangeuwawa mbele yangu namwona?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kweli kabisa
ReplyDelete