Sunday, July 19, 2015

MTOTO WA MFALME NA LULU - 3

Mfalme Mbezi alipoona kuwa walinzi wake hawarudi katika siku ileile aliyo wapangia, akaamua aongeze siku moja zaidi kuwasubiria na kama hawatafika aweze kufanya kitu ili kuhakikisha kuwa lulu ya binti yake inapatikana kwahali yoyote ile. Ilipofikia majira ya saakenda mfalme Mbezi alihisi kuwa huenda watuwake waliokuwa wamekwenda kisiwa cha mikwingwina wamep-atwa na mabaya. Akawaambia watuwake waliokuwa pamoja nae kuwa, ''Lulu kwaajili ya binti yangu nilazima ipatikane na sipo tayari kurudi Mgombezi bila lulu'' Akawaambia watu wake kuwa hakuna mtu atakayebakia ng'ambo yakisiwa cha Mikwingwina

No comments:

Post a Comment